Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo BIASHARA. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo BIASHARA. Onyesha machapisho yote

UNAHITAJI KUWA TAJIRI? Fahamu Kikwazo Ambacho Hukwamisha Wengi Kuanzisha Biashara.

NENO LA SIKU_MACHI 28/2022: UNAHITAJI KUWA TAJIRI? Fahamu Kikwazo Ambacho Hukwamisha Wengi Kuanzisha Biashara.

Hongera rafiki yangu na mfuatiliaji wa mtandao wa Fikra za Kitajiri kwa siku hii ya leo. Ni siku nyingine ambapo naamini umebahatika kuwa na siku bora, siku ambayo imekuwa ngazi ya kufikia kilele cha mafanikio unayotamani. 

Kujiunga kundi letu la WhatsApp la FIKRA ZA KITAJIRI, TAFADHALI BOFYA HAPA

Karibu tena katika makala ambazo zinalenga kukufunulia mbinu mbalimbali za kukuza pato lako.

Imekuwa ni takribani wiki tatu tangu nilipoandika makala ya mwisho ambayo ilihitimisha makundi ya biashara ambayo unaweza kuchagua kabla ya kuanzisha biashara yako.

Ikiwa hukufanikiwa kusoma mwendelezo wa makala zilizotangulia nashauri utembelee wavuti FIKRA ZA KITAJIRI ili kusoma makala zote.

SOMA: UNAHITAJI KUWA TAJIRI? Nifanye Biashara Gani Ili Kukuza Pato Langu? Sehemu ya tano.

Katika makala ya leo tutaangalia kikwazo ambacho hukwamisha watu wengi kuanzisha biashara wanazotamani. Naamini wote tunakubaliana kuwa “asilimia kubwa ya watu katika jamii wana ndoto za kuanzisha biashara”.

Iwe ni wasomi au wasiyo wasomi, wengi wanatamani kumiliki biashara kama njia mbadala ya kuingiza kipato nje ya shughuli wanazofanya.

Mwajiriwa anatamani kumiliki biashara ili awe huru kwenye kukidhi mahitaji ya kipesa.

Vivyo hivyo, mkulima au mfugaji anatamani amiliki biashara kama njia ya kujiongezea kipato nje ya shughuli zake za kilimo au ufugaji.

Ikiwa kumiliki biashara ni kiu ya watu wengi, kwa nini wengi huwa wanashindwa kuanzisha biashara?

Watu wengi wanashindwa kuanzisha biashara kwa kuendekeza kikwazo cha “kutokuwa na au uhaba wa mtaji” kama kigezo namba moja wakati wa kuanzisha biashara.

Ukiachagua watu 10 ambao wamewahi kuwa na dhamira ya kuanzisha biashara na kuwauliza kwa nini hawakufanikiwa kuanzisha biashara, watu nane wanaweza kukupatia jibu la kukosa mtaji kama kikwazo kikuu huku wengine waliobakia wakitaja vikwazo vingine nje ya mtaji.

Tafsiri yake ni kwamba, asilimia kubwa ya watu ambao wameshindwa kuanzisha biashara za ndoto zao hutanguliza mtaji kama hitaji nambari moja wakati wa kuanzisha biashara.

Hivi ni kweli kuwa mtaji ni hitaji pekee wakati wa kuanzisha biashara?

Kujibu swali hili tunatakiwa kwanza kuelewa maana ya mtaji katika mantiki ya uanzishwaji na usimamizi wa biashara.

Katika mtazamo wa biashara tunaweza kuelezea mtaji kama: “uwezo (kifedha, nguvukazi, au ujuzi) wa kuanzisha biashara, kufadhili fursa za ukuaji wa biashara, au kuzindua bidhaa mpya sokoni.”

Jambo la msingi la kuzingatia katika maana hii ya mtaji ni; tunapozungumzia mtaji hatumaanishi uwezo wa kipesa pekee!

Siyo biashara zote ambazo ni lazima uanze na kigezo cha kukosa mtaji wa kifedha, kuna biashara ambazo unaweza kuanzisha kwa kutumia nguvu kazi au ujuzi na maarifa uliyonayo.

Unaweza kutumia nguvu na maarifa au ujuzi wako kukuza uwezo wa kifedha ambao utakuwezesha kupanua biashara unayofanya katika kuelekea kwenye biashara ya ndoto yako.

Kwa mtazamo huu, tunaweza kuona kuwa watu wengi wanashindwa kuanzisha biashara kwa kutafsiri mtaji katika upande mmoja wa uwezo wa kifedha.

Tafsiri hii hupelekea wengi kushindwa kuona uwezo walionao (nguvu, maarifa au ujuzi) katika kuelekea kwenye biashara wanazotaka kuanzisha.

Pia, asilimia kubwa ya watu wanaoendekeza kiwazo cha mtaji wa kifedha, wakiulizwa swali ni kiasi gani cha mtaji wanataka na kiasi hicho kitatumika vipi katika kuanzisha biashara wanazotamani, utashangaa kuona siyo wote wanaojua kiasi kamili cha mtaji na mtiririko wa matumizi ya kiasi hiko wakati wa kuanzisha biashara.

Hali hii inatoa picha kuwa, asilimia kubwa ya watu wanashindwa kuanzisha biashara kutokana na kikwazo cha kukosa wazo na maarifa sahihi kuhusu biashara badala ya mtaji kama inavyodhaniwa.

Kwa kukosa wazo na maarifa sahihi, hupelekea wengi wawe na mtazamo wa kuanzisha biashara yenye kuhitaji mtaji mkubwa wa kipesa kabla ya kufikiria kwanza biashara ambazo mtaji wake upo ndani ya uwezo wao.

Kumbe, unapofikiria kuanzisha biashara kabla ya kusema sina mtaji ni vyema ujitathimini una uwezo gani ambao ni mtaji wa kukuwezesha kukuza mtaji zaidi wa kipesa.

Jiulize unamiliki rasilimali zipi ambazo unaweza kuzibadilisha katika mtaji wa kifedha! Jiulize una ujuzi au maarifa yapi ambayo yanaweza kutumika kukuza mtaji unaotaka!

Jiulize ni biashara ipi ambayo unaweza kuifanya kulingana na uwezo wako wa sasa! Jiulize unaweza kutumia vipi mahusiano na watu wako wa karibu katika kukuza mtaji wa biashara unayotamani.

Hitimisho. Kuna msemo kuwa "Watu hawana mpango wa kushindwa, wanashindwa kutokana na kukosa kupanga."

Unapofikiria kuanzisha biashara unatakiwa uweke mpango mzuri ambao utakuwezesha kutumia uwezo ulionao kwa sasa kama mtaji nambari moja wa kuanzisha na kukuza biashara yako.

Husiogope kuanza kidogo badala yake ogopa kutokuanzisha kile ambacho kipo ndani ya uwezo wako.


NB. Wasiliana nami kwa ajili ya kupata mwongozo kwenye masuala ya udhibiti, bajeti na uwekezaji wa pesa zako kupitia WhatsApp +255 786 881 155.


WAHI SASA UJIPATIE NAKALA YA KITABU CHA MAISHA YENYE THAMANI 

Kitabu hiki kipatikana kwa bei ya punguzo ya Tshs. 10,000/= tu! Utatumiwa kwa barua pepe au WhatsApp Nakala tete (soft copy) yenye fomati ya Pdf.


Kupata kitabu hiki, lipia kupitia Mpesa kwenye namba +255 (0) 763 745 451 au Airtel Money namba +255 (0) 786 881 155 au Halopesa namba +255 (0) 629 078 410 zote majina ni AUGUSTINE MATHIAS MUGENYI.


UNAHITAJI KUWA TAJIRI? Nifanye Biashara Gani Ili Kukuza Pato Langu? Sehemu ya Pili

NENO LA SIKU_MACHI 17/2022: UNAHITAJI KUWA TAJIRI? Nifanye Biashara Gani Ili Kukuza Pato Langu? Sehemu ya Pili.

Habari rafiki yangu na mfuatiliaji wa masomo ya Mtandao wa Fikra za Kitajiri. Ni fahari kwangu kuona unaendelea kujifunza masomo mahsusi yanayolenga kubadilisha maisha yako.

Mtandao wa Fikra za Kitajiri umedhamiria kukuletea masomo yatakayo badilisha maisha yako kwa ujumla ikiwa hata hivyo utaamua kuweka masomo haya katika vitendo kupitia maisha yako ya kila siku. 

Kujiunga kundi letu la WhatsApp la FIKRA ZA KITAJIRI, TAFADHALI BOFYA HAPA

Karibu katika makala ya leo ambayo ni mwendelezo wa masomo kuhusu jinsi unavyoweza kukuza kipato chako na hatimaye kutengeneza utajiri wa ndoto zako.

Katika makala ya jana tulijifunza kuhusu umuhimu wa kufanya tathimini kuhusu soko unalolilenga kabla ya kuingiza bidhaa au huduma kwenye soko husika.

Tuliona umuhimu wa kuchagua sehemu sahihi sambamba na kuhakikisha unaingiza sokoni bidhaa au huduma inayokidhi mahitaji ya nyakati au teknolojia katika soko husika. Kusoma mfululizo wa makala zilizotangulia  tembelea wavuti yetu ya FIKRA ZA KITAJIRI.

SOMA: UNAHITAJI KUWA TAJIRI? Nifanye Biashara Gani Ili Kukuza Pato Langu? Sehemu ya Kwanza.

Katika makala ya leo inafungua mfululizo wa makala zinazoelezea makundi ya biashara ambayo unaweza kuchagua kama njia mbadala ya kukuza pato lako.

Ieleweke kuwa kabla ya kufanya biashara yoyote ni vyema uhakikishe unawekeza zaidi kwenye kujifunza kuhusu biashara husika.

Zipo biashara ambazo zinahitaji ujuzi au ustadi maalumu; zipo biashara ambazo unalazimika kufahamu muundo wa jinsi gani zinafanya kazi; kuna biashara ambazo unalazimika kufahamu mzunguko wa uzalishaji na usambazaji wa bidhaa/huduma; kuna biashara ambazo unatakiwa kujiridisha kwenye uhakika wa upatikanaji wa malighafi au bidhaa; zipo biashara ambazo unatakiwa kufahamu kanuni na sheria na sheria maalumu zinazoongoza utaratibu wa kuendesha biashara husika kisheria; na zipo biashara ambazo unatakiwa kujua mtazamo, mila na tamaduni za wateja unaowalenga (targeted customer). 

Baada ya kujifunza kwa mapana kuhusu biashara yako na soko lake, hapa chini nakushirikisha la kwanza la biashara ambapo miongoni mwa biashara katika kundi hilo unaweza kuchagua mojawapo ya biashara inayokufaa:-

Biashara zinazo husiana na utoaji huduma (Service related business). Hili ni kundi la biashara ambalo linahusisha utoaji huduma katika soko ambalo umechagua.

Kila mtu ana ujuzi au kipaji ambacho ni cha thamani kubwa kwa wengine pale ambapo ujuzi au kipaji hicho hutumika kutatua changamoto za watu katika eneo linalokuzunguka.

Kwa ujumla, kundi hili linahusisha biashara zote ambazo zinauza rasilimali au vitu ambavyo havishikiki (non-tangible property).

Mfano, biashara ya ‘saloon’ za kike au kiume; huduma za masaji ya mwili; huduma za mazoezi ya viungo; ushauri wa kitaalamu ambao unaweza kutolewa ana kwa ana au kwa njia ya simu au mtandao; huduma ya ufundi magari, TV/Radio au ushonaji; huduma za usafi majumbani au kwenye taasisi; huduma za utunzaji wa watoto au wazee (child or elder care); huduma za elimu ya awali, msingi, sekondari au vyuo; na huduma za kwenye matukio (kupamba kumbi za sherehe, upigaji picha au video, kusherehesha, kuimba, kukodisha kumbi, magari au vifaa vya matukio ya kijamii); au huduma za usafirishaji. 

Faida. Zipo faida nyingi za biashara zinazo husiana na utoaji huduma na miongoni mwa faida hizo ni pamoja na;  

Mtaji mdogo. Baadhi ya biashara za utoaji huduma hazihitaji mtaji mkubwa wa kuanzisha biashara. Baadhi ya biashara hizi siyo lazima uwe na pango au kujenga jengo kama ilivyo kwenye biashara nyingine za viwanda.

Mtaji mkubwa wa biashara hizi ni kipaji, ustadi, ujuzi au maarifa na wakati mwingine gharama za kujitangaza. Hata hivyo, zipo biashara za utoaji huduma ambazo utalazimika kuwa sehemu maalumu ya biashara kulingana na aina ya huduma unayotoa. 

Gharama ndogo za uzalishaji. Sio lazima kutengeneza bidhaa hivyo hakuna gharama zinazotokana na mabadiliko ya bei za kununua malighafi.

Pia, baadhi ya biashara siyo lazima ukaguliwe na mamlaka za serikali kama sehemu ya kudhibiti viwango vya huduma zako.

Mara nyingi ili kulinda ubora wako katika soko mdhibiti mkubwa wa viwango vya huduma unazotoa ni wewe mwenyewe.

Urahisi wa kutoa huduma kulingana na mahitaji ya mteja. Tofauti na biashara nyingine, biashara ya utoaji huduma inaweza kubadilishwa kwa urahisi kulingana na  matakwa ya mteja.

Kwa mfano, biashara ya saloon ya kike inaweza kubadilisha mitindo ya kusuka kulingana na mahitaji ya wateja wake kwa wakati husika. Vivyo hivyo, upambaji wa kumbi utabadilika kulingana na aina ya tukio au mahitaji ya mteja.

Urahisi wa kuongeza mauzo kutokana na hisia za wateja. Moja ya sifa bora kuhusu biashara za huduma ni kwamba zinaweza kuanzishwa katika sekta yoyote au eneo lolote.

Tafsiri yake ni kwamba ni rahisi kupata fursa zinazoendana na hisia za wateja katika soko lako. Kadri unavyotoa huduma bora kwa wateja ndivyo unateka hisia za wateja wako na kufanikiwa kueneza sifa zako kwenye soko lako. 

Ni njia ya kutumia kipaji au ujuzi wako kukuza kipato chako. Kwa kuwa ujasiriamali wa utoaji huduma mara nyingi unahusu kuuza ujuzi, ustadi, maarifa au kipaji chako badala ya bidhaa halisi au vitu, ni njia ya kukuza kipato kutokana karama ulizojaliwa.

Katika makundi mengine ya biashara mara nyingi unalazimika kuanza na mtaji wa pesa hila kwenye utoaji huduma unaweza kuanza kukuza mtaji kwa kutumia kipaji chako.

Mfano, kuna vijana wengi ambao nawafahamu wamefanikiwa kukuza mitaji yao na kuwekeza kwenye biashara nyingine kupitia huduma ya kusafisha na kuweka urembo wa kucha za akina mama. Hivyo, katika utoaji huduma mtaji wa kwanza ni kipaji, ujuzi, ustadi au maarifa yako.

Biashara katika kundi hili haziathiriwi sana na mfumuko wa bei. Faida nyingine muhimu ya biashara za huduma ni kwamba haziathiriwi sana na kushuka kwa uchumi ikilinganishwa na biashara za bidhaa.

Wafanyabiashara wanaotoa huduma pia wana uwezekano mkubwa wa kulinda bei za huduma zao au kupandisha bei wenyewe maana biashara nyingi katika kundi hili zinahusisha maelewano ya mtoa huduma na mteja wake.

Changamoto za kufanya biashara za utoaji huduma. Zipo changamoto kadhaa ambazo zinakabiri biashara za utoaji huduma na miongoni mwa changamoto hizo ni:

  • Huduma hazionekani au kushikika - hali hii husababisha ugumu wa kuingia sokoni kwa wafanyabiashara wapya; 
  • Huduma haziwezi kutenganishwa na watoa huduma - hali hii husababisha ugumu wa usambazaji huduma kwa wateja (Mfano, msusi ni lazima afanye kazi ya ususi ili aingize kipato); 
  • Ujuzi, ustadi, maarifa au kipaji - Mbali na hayo, wajasiriamali wanatakiwa kuhakikisha kuwa wana ujuzi na mafunzo sahihi au kipaji cha kutoa huduma bora kwa wateja katika soko lao; 
  • Huduma kwa wateja - Ili uendeleze biashara ya utoaji huduma ni lazima ulinde viwango, ubora, ubunifu na kauli kwa wateja wako. Mara zote unatakiwa kujikita kwenye kutatua changamoto za wateja wako kwa viwango vya juu, hii ni tofauti na biashara ya bidhaa maana kuna bidhaa ambazo zinajiuza zenyewe kutokana na ubora wake kwenye soko. 
Hitimisho. Biashara ya utoaji huduma ni fursa hai kwa kila mtu kutokana na urahisi wa kuanzisha biashara hii kuanzia kwenye hatua za chini.

Ili kufaidika na biashara katika kundi hili unachotakiwa kufanya ni kujiuliza una ujuzi, ustadi, kipaji au maarifa yapi ambayo yanaweza kutumika kutatua changamoto za watu katika jamii inayokuzunguka.

Baada ya kugundua uwezo uliopo ndani mwako, hatua inayofuata ni kuanza kutoa huduma kwa jamii inayokuzunguka.

Wakati mwingine unaweza kuanza kutoka huduma bila malipo kama njia ya kutangaza uwezo ulioko ndani wako. Anza sasa na kumbuka kunishukuru baada ya kuona matokeo!

NB. Wasiliana nami kwa ajili ya kupata mwongozo kwenye masuala ya udhibiti, bajeti na uwekezaji wa pesa zako kupitia WhatsApp +255 786 881 155.


WAHI SASA UJIPATIE NAKALA YA KITABU CHA MAISHA YENYE THAMANI 

Kitabu hiki bado kinatolewa kwa bei ya OFA kwa kuchangia cha Tshs. 10,000/= tu! Utatumiwa kwa barua pepe au WhatsApp Nakala tete (soft copy) yenye fomati ya Pdf.


Kupata kitabu hiki, lipia kupitia Mpesa kwenye namba +255 (0) 763 745 451 au Airtel Money namba +255 (0) 786 881 155 au Halopesa namba +255 (0) 629 078 410 zote majina ni AUGUSTINE MATHIAS MUGENYI.




UNAHITAJI KUWA TAJIRI? Nifanye Biashara Gani Ili Kukuza Pato Langu? Sehemu ya Kwanza.

NENO LA SIKU_MACHI 15/2022: UNAHITAJI KUWA TAJIRI? Nifanye Biashara Gani Ili Kukuza Pato Langu? Sehemu ya Kwanza.

Hongera rafiki yangu kwa siku hii ya leo ambayo naamini imekuwa msingi wa kupiga hatua moja kuelekea mafanikio ya ndoto za maisha yako.

Kujiunga kundi letu la WhatsApp la FIKRA ZA KITAJIRI, TAFADHALI BOFYA HAPA

Karibu katika makala ya leo ambayo ni mwendelezo wa kujifunza kuhusu mbinu ambazo zitakuwezesha kukuza pato lako na hatimaye kufikia utajiri wa ndoto zako.

Ni mafundisho ambayo yamedhamiria kubadilisha maisha ya kila mtu ambaye amedhamiria kujifunza na kuweka mafundisho katika vitendo kupitia maisha yake ya kila siku. 

Hakikisha unafuatilia makala zilizopita kwa kutembelea wavuti yetu ya FIKRA ZA KITAJIRI.


Watu wengi wana ndoto za kufanya biashara lakini wanashindwa kuchagua aina ya biashara ambayo itakuwa endelevu na kukidhi mahitaji yao. 

Kwa kukosa mwongozo sahihi wakati wa kuchagua aina biashara, wengi wamejikuta wakianzisha biashara ambazo zinakufa ndani ya muda mfupi. 

Tafiti zinaonyesha kuwa asilimia 80 ya biashara zinazoanzishwa huwa zinakufa ndani ya kipindi cha miaka mitano.  

Hata zile ambazo hufanikiwa kupenya kipindi hicho, nyingi huwa zinaendeshwa kwa hasara pasipo kuzalisha faida kinyume na makadirio ya wamiliki wa biashara husika. 

Tafsiri yake nini? Tafiti hizo zinatupa mwanga wa juu ya idadi kubwa ya watu ambao wanaanzisha biashara bila kufanya tafiti za kutosha au kuanzisha biashara katika eneo na nyakati zisizo sahihi. Ndiyo! Pigia msitari maneno eneo na nyakati sahihi.

Katika biashara, eneo na nyakati sahihi ni maneno yanayobeba sifa za soko la biashara unayokusudia kuanzisha. 

Kuhusu eneo sahihi, Siyo kila biashara unaweza kuifanya katika kila eneo. Wengi kutokana na kutokufanya tafiti za kutosha au kwa kuigizia biashara hujikuta wanaanzisha biashara katika maeneo ambayo siyo sahihi kwa biashara husika. 

Tafsiri yake ni kwamba biashara nyingi zinakufa kutokana na kuanzishwa katika soko ambalo siyo sahihi. 

Hivyo, kabla ya kuanzisha biashara unatakiwa kufanya tathimini ya soko. 

Jiulize ikiwa bidhaa au huduma unayotaka kuiweka sokoni kama inakidhi mahitaji ya soko husika. 

Jiulize katika soko hilo bidhaa au huduma yako inalenga kutatua changamoto ipi na kwa kundi lipi. 

Wafanyabiashara wengi huwa wanaangukia kwenye mtego huu kwa kushindwa kutambua soko wanalolenga katika eneo husika. 

Hali hii hupelekea wengi kuingia katika soko na bidhaa au huduma ambazo hazihitajiki kwa wingi kwa vile zinatatua changamoto za idadi ndogo ya watu katika jamii (soko) husika.

Kuhusu nyakati sahihi, hiki ni kigezo kingine cha kulipima soko lako. 

Je, bidhaa au huduma unayotaka kuiweka sokoni inaendana na mahitaji ya wateja kwa nyakati husika? 

Je, mbinu unazotaka kutumia kwenye uzalishaji, mauzo na usambazaji wa bidhaa au huduma husika zinaendana na matakwa ya nyakati husika? 

Teknolojia ibadilika kila siku, biashara ilifanya vizuri miaka mitano iliyopita inaweza isifanye vizuri kwa sasa. 

Mfano, kuna watu mpaka sasa wanakomaa na biashara ya kukodisha CD za filamu au kuingiza miziki kwenye simu, wakati kwa teknolojia ya wakati huu kila mtu anaweza kupata nyimbo au filamu anayotaka kutoka kwenye mtandao. 

Fikiria baadhi ya wafanyabiashara ambao hadi sasa wanakomaa na biashara ya 'internet cafe' wakati ulimwengu wa karne hii asilimia kubwa ya watu wanatembea na huduma hiyo mikononi. 

Fikiria katika karne hii mtu ambaye anaanzisha biashara ya kuuza magazeti wakati asilimia kubwa ya watu wanasomo magazeti kupitia simu janja. 

Ninachotaka hapa ujifunze ni kwamba, kabla ya kufungua biashara hakikisha mbinu za uzalishaji, mauzo na usambazaji zinaendana na matakwa ya nyakati hizi. 

Pia, unatakiwa kubadilisha mbinu za biashara yako au kubadilisha biashara kabisa kadri teknolojia inavyobadilika.

Hitimisho. Kila mtu anaweza kuanzisha biashara lakini siyo biashara zote zitakuwa endelevu. 

Unapoamua kuanzisha biashara husikurupuke kutokana na taarifa za juu kuhusu faida ya bidhaa au huduma husika katika soko. 

Unaweza kuhadithiwa mazuri ya bidhaa au huduma kwenye soko lakini pengine yote uliyohadithiwa yakashindwa kuonekana katika soko unalolilenga. 

Mara zote kabla ya kuweka bidhaa au huduma kwenye soko hakikisha una tafiti za kutosha kuhusu soko hilo.

NB. Wasiliana nami kwa ajili ya kupata mwongozo kwenye masuala ya udhibiti, bajeti na uwekezaji wa pesa zako kupitia WhatsApp +255 786 881 155.


WAHI SASA UJIPATIE NAKALA YA KITABU CHA MAISHA YENYE THAMANI 

Kitabu hiki bado kinatolewa kwa bei ya OFA kwa kuchangia cha Tshs. 10,000/= tu! Utatumiwa kwa barua pepe au WhatsApp Nakala tete (soft copy) yenye fomati ya Pdf.


Kupata kitabu hiki, lipia kupitia Mpesa kwenye namba +255 (0) 763 745 451 au Airtel Money namba +255 (0) 786 881 155 au Halopesa namba +255 (0) 629 078 410 zote majina ni AUGUSTINE MATHIAS MUGENYI

UNAHITAJI KUWA TAJIRI? Anzisha Au Miliki Biashara Kama Njia Ya Kukuza Utajiri Wako

 NENO LA SIKU_MACHI 12/2022: UNAHITAJI KUWA TAJIRI? Anzisha Au Miliki Biashara Kama Njia Ya Kukuza Utajiri Wako 

Habari rafiki kwa kuendelea kufuatilia masomo ya Mtandao wa Fikra za Kitajiri. Hongera kwa kuwa na siku bora katika maisha yako. Naamini imekuwa ni siku bora kwako kwa kuwa umeitumia kutengeneza ushindi mdogo kwa ajili ya kuelekea kwenye kilele cha mafanikio unayotaka. 

Kujiunga kundi letu la WhatsApp la FIKRA ZA KITAJIRI, TAFADHALI BOFYA HAPA

Karibu katika makala ya leo ambapo nitakushirikisha kuhusu umuhimu wa kuanzisha au kumiliki biashara yako kama njia ya kuelekea kwenye maisha yenye uhuru wa kifedha.

Makala hizi ni mwendelezo wa makala ambazo zinakufunulia jinsi gani unaweza kutengeneza utajiri wa ndoto yako kuanzia kwenye ngazi ya chini kabisa. Ikiwa ni mara yako ya kwanza kusoma makala hizi, hakikisha unafuatilia makala zilizotangulia.

SOMA: UNAHITAJI KUWA TAJIRI? Fahamu Jinsi Ya Kukuza Pato Lako

Biashara ni njia mojawapo ya kuzalisha kipato ambayo hutumiwa na watu wengi katika jamii. Linapotajwa neno ‘biashara’ watu wengi hufikiria kuuza bidhaa au huduma za kiwango cha juu na ndio sababu wengi hukimbilia kusema hawana mtaji wa kuanzisha biashara.

Biashara ni kazi au shughuli inayohusisha ubunifu au ununuzi na uuzaji wa bidhaa au huduma kwa faida.

Hivyo, biashara inaweza kuwa kilimo, ufugaji, biashara ya duka, kusambaza bidhaa, uuzaji wa huduma, uongezaji thamani kwenye bidhaa, ufundi, usafirishaji au huduma  inayotokana na matumizi ya kipaji kwa utaratibu maalumu wa malipo.

Kwa tafsiri hii, unaweza kuona kuwa: kwa asili kila mtu ni mfanyabiashara hila tunazidiana kwenye viwango na aina za biashara ambazo tunajihusisha nazo.

Kulingana na tafsiri ya biashara hapo juu, unaweza kuona kuwa biashara inahusisha pande mbili kubalishana thamani kwa faida.

Ili biashara ikamilike ni lazima pawepo mtu anayotoa na anayepokea bidhaa au huduma kwa kubadilishana na kitu kingine. 

Hivyo, biashara inahusisha ubunifu wa kuzalisha au kununua bidhaa au huduma kwa kuzibalisha na kitu cha thamani chenye faida ikilinganishwa na gharama zilizotumika kubuni, kuzalisha bidhaa au kutoa huduma husika.

Hapa ndipo tunapata neno ‘Mjasiriamali (Entrepreneur)’, ambalo hutumika kujumuisha watu ambao hubuni na kuanzisha biashara mpya na wapo tayari kubeba hatari katika kuanzisha biashara hiyo kwa ajili ya kufurahia manufaa yatokanayo na biashara husika.

Nani anaweza kuwa Mjasiriamali? Kila mtu anaweza kuwa mjasiriamali kwa kubuni na kuanzisha biashara kwa ajili ya kujiongezea kipato. Ikiwa unahitaji kukuza utajiri wako hakuna namna nyingine zaidi ya kuhakikisha unabuni na kuanzisha au kununua bidhaa au kutoa huduma kwa faida.

Matajiri wengi ambao unawafahamu hapa Tanzania au Duniani kote, wengi wamepata utajiri huo kupitia ubunifu na uzalishaji wa bidhaa au huduma kulingana na mahitaji katika soko.

Pia, ukifuatilia zaidi matajiri wengi utagundua kuwa wengi wametengeneza utajiri wao, kwa maana, walianzia hatua za chini kabisa mpaka kufikia viwango vya kujulikana na kuliteka soko. 

Hitimisho. Je, umewahi kutamani kuanzisha au kumiliki biashara yako? Kama jibu ni ndiyo, fahamu kuwa unaweza kuwa tajiri wa kesho ikiwa umedhamiria kufuata misingi ya kutengeneza utajiri.

Tukutane katika makala ijayo ambapo nitaendelea kukufunulia maarifa muhimu kuhusu biashara kama msingi imara wa kukuza pato lako.


NB. Wasiliana nami kwa ajili ya kupata mwongozo kwenye masuala ya udhibiti, bajeti na uwekezaji wa pesa zako kupitia WhatsApp +255 786 881 155.


WAHI SASA UJIPATIE NAKALA YA KITABU CHA MAISHA YENYE THAMANI 

Kitabu hiki bado kinatolewa kwa bei ya OFA kwa kuchangia cha Tshs. 10,000/= tu! Utatumiwa kwa barua pepe au WhatsApp Nakala tete (soft copy) yenye fomati ya Pdf.


Kupata kitabu hiki, lipia kupitia Mpesa kwenye namba +255 (0) 763 745 451 au Airtel Money namba +255 (0) 786 881 155 au Halopesa namba +255 (0) 629 078 410 zote majina ni AUGUSTINE MATHIAS MUGENYI.




NENA NA NAFSI YAKO KUHUSU UTAJIRI WA NDOTO YAKO: KAULI 20 ZITAKAZOBADILISHA MTAZAMO WAKO.


   NENO LA LEO (APRILI 20, 2021): NENA NA NAFSI YAKO KUHUSU UTAJIRI WA NDOTO YAKO: KAULI 20 ZITAKAZOBADILISHA MTAZAMO WAKO.

Habari ya asubuhi rafiki yangu na mwanafamilia ya FIKRA ZA KITAJIRI. Ni asubuhi nyingine ambayo nafasi ya kukushirikisha neno la tafakari ya leo. Matumaini yangu ni kwamba umepata pumzi ya uzima na upo tayari kuendelea na majukumu yako siku ya leo. Katika neno la tafakari ya leo ambapo tutajifunza kauli 20 ambazo kila siku unatakiwa kuzinena dhidi ya nafsi yako kuhusu nguvu uliyonayo katika kuvuta utajiri unaohitaji. Tunafahamu kuwa maneno unayonena dhidi ya nafsi yako yana nafasi kubwa ya kuharibu au kujenga uwezo wako wa kujiamini katika kile unachoamini. Karibu tujifunze kwa pamoja:-

Je unahitaji kupata mafundisho ya aina hii kila siku? Jiunge kundi letu la WhatsApp la FIKRA ZA KITAJIRI, tafadhali BOFYA HAPA KUJIUNGA.

1. Mimi ni tajiri, mimi ni mwanaume/mwanamke tajiri, mimi ni sumaku nitavuta utajiri kwangu kutoka pande zote.

2. Mimi ni sehemu ya ulimwengu usio na mwisho na usio pungukiwa hivyo nimeunganishwa na kila kitu ninachohitaji katika kufikia utajiri wa ndoto yangu.

3. Nitawapa wengine thamani kubwa, kila mara nitakuwa mtu wa thamani kwa wengine, mimi ni mtu asiye na ukomo wa maoni na fikira za ubunifu. Natambua kuwa nitabarikiwa utajiri zaidi kadri ninavyotoa thamani kwa wengine.

4. Kuna zaidi ya kutosha kwa kila mtu. Wingi uko kila mahali ninapoangalia. Ninaona utajiri, wingi na ustawi kila mahali niendako.

5.   Nastahili kuwa tajiri. Utajiri ni haki yangu ya kuzaliwa. Utajiri ni sehemu ya maisha yangu. Ulimwengu upo tayari kunizawadia utajiri wa ndoto yangu.

SOMA: MAISHA YA UTAJIRI AU UMASIKINI: JE NI IPI HAKI YAKO YA KUZALIWA?

6.  Nimeumbwa kwa ajili ya kuishi maisha ya shibe, maisha ya kuwa na zaidi, maisha ya kujitosheleza. Hivyo, shibe ni haki yangu ya kuzaliwa. Sijaumbiwa maisha ya dhiki kwa kuwa Muumba anachukia dhiki kwa waja wake.

7. Ninawaombea watu wote maisha ya utajiri wa ndoto zao, maisha ya shibe. Ninanayo furaha kubwa kadri ninavyoona natumika kuwasaidia watu wengine kufikia utajiri wa ndoto zao. Upendo ni nyenzo kuu ambayo nitaendelea kuitumia kusaidia watu.

8. Mimi nimeumbwa na Mungu ambaye aliniweka katika Ulimwengu huu na kuinua nafsi yangu juu. Nimepewa mamlaka ya kutawala vitu vyote na kupitia kuumbwa kwa sura na mfano wake nimepewa mamlaka ya kuumba kila kitu ambacho nakiona katika fikra zangu.

9.   Kila siku, kwa kila njia, ninazidi kuwa tajiri. Najipima nakuona kuwa matendo yangu yananiwezesha kukua kiuchumi kila siku. Nitaendelea kuwa sehemu ya kukuza utajiri wangu kupitia matendo yangu.

10.  Hakuna ubaya wowote kuhusu pesa ikiwa pesa inapatikana na kutumika kwa njia halali. Mimi ndo nitaifanya pesa ionekane mbaya au nzuri kupitia matumizi ya pesa inayoingia mikononi mwangu.

11.  Matendo yangu yana thamani kwa wengine kiasi gani? Nitaendelea kutumia pesa kupima thamani ninayoitoa kwa wengine. Watu wapo tayari kulipia thamani ninayoitoa kwao kulingana na mahitaji ya soko.

12.  Pesa ni nishati safi ya kuniwezesha kumiliki na kuitawala dunia. Pesa inaundwa katika mfumo wangu wa fikra. Pesa iko akilini mwangu. Nitaendelea kutumia akili yangu kuvuta pesa ninazohitaji siku baada ya siku.

13. Ninastahili kumiliki pesa. Ninastahili kuwa na pesa nyingi. Hivyo, nipo tayari kuvutia kiasi kikubwa cha pesa kwangu kupitia thamani ninayoitoa kwa wengine.

14. Kuwa tajiri kunanipa nguvu ya kusaidia watu wengine wenye mahitaji katika Ulimwengu huu kwa ajili ya kufanya mabadiliko makubwa katika maisha yao. Nitatumia sehemu ya kiasi cha pesa ninachopata kwa ajili ya kukusaidia na kuinua watu wengine.

15.  Mimi ni msimamizi mkuu wa pesa yangu. Sitakubali pesa itumike kuharibu maisha yangu. Nitasimamia maisha yangu ya kifedha kwa ajili ya utakaso wa nafsi yangu katika maisha haya na maisha yajayo.

16.  Pesa inaenda sehemu ambako inapendwa na kuthaminiwa zaidi. Nitahakikisha kila shilingi inayoingia mkononi mwangu inatumika kulingana na bajeti. Nitahakikisha natumia pesa ninayoipata kukuza uwezo wangu wa kifedha kwa kuhakikisha pesa inatumika kuzalisha pesa zaidi.

KUJIUNGA NA PROGRAMU MAALUM YA "JILIPE KWANZA": SOMA MAKALA HII KWA KUBONYEZA MAANDISHI HAYA YENYE RANGI

17.  Natambua kuwa kiwango cha pesa ninachopata kina uhusiano mkubwa na kiwango cha pesa ninachotoa kwa wengine. Kadiri ninavyotoa zaidi, ndivyo ninavyozidi kuwa tajiri. Kadiri ninavyotoa zaidi ndivyo nazidi kuunganishwa na watu ambao watanifungulia milango ya kukua zaidi kiuchumi.

18.  Watu wanaonizunguka wanabariki utajiri wangu kwa maana nimekuwa wa msaada kwao katika kila hali. Nimekuwa mtu wa kufunua fursa kwa wengine. Nimekuwa mtu wa kuendelea kuhamasisha wengine. Nimekuwa mtu wa kuonesha wengine kuwa kila jambo linawezekana.

19. Ninapumua kwa raha. Naendelea kuwa sehemu ya jamii inayolinda ubora wa hewa tunayovuta. Kila pumzi ninayovuta huongeza ufahamu wangu kuhusu wingi unaonizunguka.

20.  Nina fikra za kimilionea. Nina mawazo kimilionea. Natenda kama milionea, nahisi kama milionea, mimi ni milionea. Ninashinda vizuizi vyote ambavyo viko katika njia yangu ya mafanikio na uhuru wa kifedha.

Mwisho, katika neno la tafakari ya leo nimekushirikisha kauli 20 kutoka kwenye vyanzo tofauti ambavyo vimeandika kuhusu utajiri. Hizi ni kauli chache ambazo unaweza kuzinena dhidi ya nafsi yako katika maisha yako ya kila siku. Unaweza kurekebisha au kuboresha kauli hizo ili ziendane na mazingira ya maisha yako. Kumbuka, mbegu ikidondoka ardhini ni lazima iote na kuzaa matunda, nami naiombea mbegu hii niliyodondosha kupitia neno la tafakari ya leo ipate kuzaa matunda mengi katika Maisha yako.

PS: Unaweza kujipatia maarifa kwenye elimu ya pesa kupitia usomaji wa vitabu. Chagua nakala za uchambuzi wa vitabu unavyotaka kwa kubofya kiunganishi hapo chini. Kila nakala ya uchambuzi wa kitabu inapatikana kwa gharama ya Tshs. 3,999. Wahi mapema OFA hii.

πŸ‘‡πŸΎπŸ‘‡πŸΎπŸ‘‡πŸΎπŸ‘‡πŸΎπŸ‘‡πŸΎ

BOFYA HAPA KUPATA ORODHA YA UCHAMBUZI WA VITABU

 

BORN TO WIN ~ DREAM BIG

Mwalimu Augustine Mathias

Mawasiliano: 0763 745 451/0786 881 155/0629 078 410

Barua pepe: fikrazakitajiri@gmail.com