Mambo Niliyojifunza Kwenye Kitabu cha Everything I Know About Sales Success: Mbinu muhimu za kuwa muuzaji bora


Habari ya leo rafiki na msomaji wa mtandao wa fikra za kitajiri.

Ni muda mrefu tangu nimekushirikisha makala za vitabu ninavyosoma kila wiki hali ambayo ilisababishwa na kushiriki mafunzo maalumu ya kazi yangu ambayo yaliniweka nje ya mtandao kwa muda.

Pamoja na hayo bado ni nina hali ya kuendelea kukushirikisha yale ninayojifunza ili kwa pamoja tuendeleze jitihada za kuboresha maisha yetu. Karibu tena katika mtandao wa FIKRA ZA KITAJIRI kwa uchambuzi wa kitabu cha wiki hii.

Kujiunga na mtandao huu, KWA KUBONYEZA BONYEZA HAPA na kujaza fomu kisha bofya “jiunge/subscribe” utakuwa umejiunga na mtandao huu. Kwa kujiunga na mtandao huu utapata makala zinazochapishwa humu moja kwa moja kwenye barua pepe yako bila malipo yoyote.

Kitabu cha wiki hii ni Everything I Know About Sales Successkutoka kwa mwandishi Gerhard Gschwandtner. Kupitia kitabu hiki mwandishi anatushirikisha mbinu muhimu ambazo zimetumiwa na watu mbalimbali waliofanikiwa kwenye tasnia ya mauzo ya bidhaa/huduma za kampuni zao. Watu hawa wengi wao walianzia ngazi ya chini na pengine bila kusomea kozi ya mauzo lakini kupitia nia na dira maalumu walifanikiwa kufikia ngazi za juu kabisa.

Karibu tujifunze machache kati ya mengi ambayo mwandishi anatushirikisha katika kitabu hiki:

1. Mwandishi anatushirikisha kuwa siri kubwa katika mauzo ni kufahamu kuwa unafanikiwa kimauzo pale tu unapowasaidia watu kupata kile wanachohitaji au kutatua matatizo yao. Kwa ufupi tunaweza kusema ni kuwaridhisha wateja kwa kupata kile wanachotaka. Na hapa ndipo mwandishi anatushirikisha kuwa mafanikio ya kimauzo hayapimwi kwa kuangalia mauzo tu bali kwa kuangalia mahusiano muhusika alionayo na wateja wake au jamii inayomzunguka kwa ujumla.

2. Taarifa sahihi na kwa wakati sahihi ni nyenzo muhimu ambayo muuzaji bora anatakiwa kuwa nayo. Nyenzo hii inahusisha taarifa muhimu za masoko mapya, taarifa za uendeshaji wa biashara/kampuni, taarifa za teknolojia mpya au taarifa za kiubunifu kwenye uzalishaji wa bidhaa/huduma mpya. Siri hii imetumiwa na makampuni mengi kutumia teknolojia mpya au masoko mapya katika nchi zinazoendelea kufikia mafanikio makubwa.

3. Tengeneza timu ya watu wenye uchu wa kufanikiwa kimauzo. Mwandishi anatushirikisha kuwa mauzo yanategemea timu ya watu hivyo kama ni kampuni hakikisha unazungukwa na watu wenye uchu wa kufanikiwa kimauzo. Hii ni pamoja na kuwa na timu ya wafanyakazi ambao ni waaminifu kwa kampuni ikiwa ni pamoja na kila mmoja kwenye kampuni husika kumiliki hisa za kampuni. Pale mfanyakazi anapomiliki hisa za kampuni anakuwa ni sehemu ya wamiliki wa kampuni jambo ambalo litapelekea afanye kazi kwa weledi ili kufanikisha maendeleo ya kampuni. Kwa ujumla unahitaji kuwa na timu ya watu ambao wapo tayari kujiongoza katika majukumu yao na kufanya kazi kwa ubunifu na weledi.

4. Safari ya mafanikio kimauzo inaanza na maneno ya kukatishwa tamaa kutoka watu/jamii inayokuzunguka. Mwandishi anatushirikisha kuwa wote waliofanikiwa wamepitia kwenye hali ambayo kila mmoja wetu ambaye anathubutu kufanikiwa kimauzo. Silaha muhimu ambazo unatakiwa kuwa nazo ni kufahamu nini unataka kupata na kwa muda gani (lini). Unahitaji kuchora mstari wako wa mafanikio ya kimauzo na kuanza kuutekeleza mara moja. Hapa unahitaji kuwa na sifa ya uvumilivu, bidii ya kazi, uchu wa kusonga/kupata zaidi na kuendelea kwenye imani ya kile unachoamini katika kufikia ngazi ya mafanikio ya ndoto zako.


5. Dhibiti kila shilingi inayoingia na kutoka katika biashara yako. Uhai wa biashara yoyote unategemea namna ambavyo fedha inayoingia na kutoka inavyodhibitiwa. Mwandishi anatushirikisha kuwa ni lazima kudhibiti fedha zinatoka hasa pale ambapo tunafanya manununizi/matumizi kwa ajili ya biashara lakini pia kuhakikisha kuwa fedha inayoingia kwenye biashara kupitia mauzo inakuwa na thamani zaidi ya ile iliyowekezwa. Kwa ufupi ni kwamba ni lazima uwe tayari kununua na kuuza kwa faida ikiwa ni pamoja na kudhibiti matumizi yasiyo na mpangilio.

6. Mafanikio ya mauzo yanaanzia kwenye kuwekeza muda wa kutosha kwa ajili ya maandalizi na kupanga mipango ya baadae. Ili uuze ni lazima uwe na bidhaa au huduma ambayo wewe mwenye unaridhika nayo. Mwandishi anatushirikisha kuwa kama unahitaji kuongeza mauzo ni lazima ujiulize maswali haya: Je kila siku natenga muda kiasi gani kwa ajili ya kuandaa mauzo ya siku inayofuata? Je kila siku unajiwekea malengo kwa ajili ya mauzo ya siku husika ikiwa ni pamoja na kuandaa orodha ya majukumu ya siku husika? na Je una mkakati maalum kwa ajili ya kuwa na bidhaa/huduma bora zaidi kuliko wapinzani wako kibiashara? Kwa ujumla utagundua kuwa maswali haya yote yanakuhitaji kuwekeza muda wa kutosha kwa ajili ya kuboresha biashara yako.

7. Kufanikiwa kimauzo ni lazima uwe na sifa kuu tatu ambazo ni: shauku ya kufanikiwa; ufahamu wa watu/jamii unayofanya nayo kazi; na ufahamu wa kutosha juu ya huduma au bidhaa ambayo unauza. Hizo ni sifa kuu tatu za kufanikiwa kimauzo ambazo mwandishi anatushirikisha kutoka kwa mwanamafanikio nguli Donald Trump ambaye kwa sasa ni rais wa Marekani. Jiulize je una shauku na bidhaa/huduma ya biashara yako?; je upo tayari kubadilisha mfumo wa mauzo kwa kutegemea aina ya watu unaofanya nao kazi? na Je unaweza kubuni njia mbadala kwa ajili ya kuboresha bidhaa au huduma yako?.

8. Katika ulimwengu wa mauzo ni lazima utambue kuwa hakuna njia moja sahihi au ya kipekee ya kufikia lengo. Kutokana na ukweli huu ni lazima kila siku uwekeze kwenye kutafuta mawazo mapya kwa ajili ya kuboresha mfumo wako wa mauzo. Kuwa tayari kufuta mifumo ya zamani ambayo yanaonekana kutokwenda na nyakati. Kwa ujumla tambua kuwa hakuna njia sahihi au hisiyo sahihi ya kufikia lengo lako la kimauzo.

9. Kufanikiwa kimauzo unatakiwa kutambuwa kuwa kukataliwa ni sehemu ya kukujenga na hivyo kadri unavyokataliwa ndivyo unakua zaidi katika ulimwengu wa mauzo. Hapa unahitaji kuachana na roho ya kukatishwa tamaa na badala yake wekeza muda wako kusonga mbele zaidi. Pia, unahitaji kutambua kuwa nyakati ngumu kimauzo hazitakiwi kukuzuia kuendelea kufikiria kwa mapana zaidi. Fikiria kufanikiwa zaidi, kufikiria kufanya maamuzi sahihi na fikiria kuwa bora zaidi.

10. Ubunifu wa mara kwa mara ni injini ya kukuza mauzo katika biashara. Ubunifu huu ni lazima ujikite kwenye uboreshaji wa bidhaa/huduma zinazotolewa kwa wateja kulingana na nyakati husika. Mwandishi anatushirikisha kuwa biashara bila ubunifu wa mara kwa mara kamwe haiwezi kuendelea na badala yake itadumaa siku zote na mwisho wake ni kushuka kwa mauzo. Hili ni tatizo kubwa ambalo linakumba wafanyabiashara wa kati walio wengi katika mazingira yanayotuzunguka.

11. Mara zote katika biashara lenga kuzalisha/kuendesha biashara kwa gharama ya chini ili uingie sokoni kwa bei nafuu. Hata hivyo, pamoja na kuzalisha au kujiendesha kwa gharama nafuu unatakiwa kulinda ubora wa bidhaa/huduma zako. Mwandishi anatushirikisha kuwa kadri unavyozalisha kwa gharama nafuu ndivyo unavyomfikia mteja kwa gharama ambazo hazimuumizi sana. Na hii ni nyenzo muhimu ya kuwashinda wapinzani wako kibiashara.  

12. Kuwa na utamaduni wa kusikiliza mrejesho wa wateja dhidi ya bidhaa au huduma zako. Mwandishi anatushirikisha kuwa mauzo hayaishii pale unapouza bidhaa/huduma yako kwa mteja bali pale mteja anaporidhika na bidhaa/huduma yako. Lazima uwe tayari kutenga gharama kwa ajili ya kurekebisha au kubadilisha bidhaa ambazo zimeingizwa sokoni zikiwa chini ya ubora. Hii ni pamoja na kuweka muda wa uhakika (warranty/guarantee) kwa mteja kutumia bidhaa kwa kipindi flani pasipo kupata hitilafu yoyote ya kiufundi. Pia, unaweza kuweka utaratibu wa huduma ya simu ya bure kwa wateja ili kupata mrejesho wao dhidi ya bidhaa/huduma zako.  

13. Kama mtendaji mkuu wa biashara au kampuni yako, kazi kubwa ulionayo ni kuhakikisha unaonesha mwelekeo wa malengo ya kampuni au biashara husika. Hii ni pamoja na kuhakikisha kuwa kila mmoja ndani ya timu yako anafahamu mwelekeo wako na hatimaye hakikisha kuwa wote wanafanya kazi kufikia mwelekeo husika.

14. Hizi ni baadhi ya sifa za kufanikiwa kimauzo ambazo mwandishi anatushirikisha kutoka kwa mwanamafanikio Arnold Schwarzenegger: Kwanza kabisa ni lazima uchore mstari wako wa mafanikio – tambua ni wapi unataka kufikia kimafanikio; mbili, kataa kila aina ya vikwazo – kuwa na imani hisiyo kuwa na chembe ya shaka juu ya ndoto yako ya mafanikio na hivyo kuwa tayari kukataa kila aina ya vikwazo mbele ya safari yako; tatu, lenga kuwa bora kuliko wote katika kile ambacho umekusudia kufanya; nne, kumbuka ni lazima kujitoa kwa nguvu zako zote – husitegemee vitu kutokea kama muujiza bali ni lazima ujione kuwa wewe ndio mhusika mkuu wa kufanya miujiza hiyo itokee; tano, husikubali k ushindwa – tambua kuwa kuna kupanda na kushuka katika safari yako hivyo mara zote nyakati za kushuka zikufundishe kitu kwa ajili kupanda juu zaidi; sita, tumia ushawishi/kukubalika kwako ajili ya kwenda hatua ya ziada – Arnold baada ya kuona amefanikiwa kwenye tasnia ya filamu alihamia kwenye siasa ambako nako alifanikiwa kuchaguliwa kama Gavana wa California; na mwisho waoneshe watu kuwa kila unapoweka malengo ya juu huwa unayafikia kupitia matendo yako.

15. Kufanikiwa kimauzo ni lazima uwe tayari kudhibiti hisia zako. Kumbuka kuwa tasnia ya mauzo inakuunganisha na watu mbalimbali tena wenye mitazamo taofauti. Katika kila hali ni lazima ukubali kuruhusu mantiki (logic) itumike badala ya hisia (feelings) katika kila maamuzi unayofanya. Unahitaji kujifunza kusikiliza zaidi kuliko kuwa mzungumzaji mkuu – kuwa tayari kuhimili hisia za wateja/jamii inayokuzunguka tena kwa busara na hekima ya hali ya juu.  

16. Kuongeza idadi ya mteja ni lazima uhakikishe kila mtu unamchukulia kama mteja tarajiwa wa bidhaa/huduma zako. Mwandishi anatushirikisha kuwa kila unapokutana na watu wapya katika maisha hakikisha unaongea nao kana kwamba unaongea na wateja wako au wateja tarajiwa. Hapa unahitaji kuwa na nyuso za furaha na tabasamu kila mara unapokutana na watu wapya.

17. Kumbuka kurejesha kwenye jamii. Mwandishi anatushirikisha kurudhisha kwenye jamii ni sehemu ya kukua kimauzo kutokana na ukweli kwamba kadri unavyojiweka karibu na jamii ndivyo biashara zako zinavyopendwa zaidi. Hapa unahitaji kutenga sehemu ya faida yako kwa ajili kuwekeza kwenye shughuli za kijamii. Tenga sehemu ya faida yako kwa ajili ya wahitaji katika jamii kama vile watoto yatima, wajane na wazee wenye mahitaji maalumu.

18. Mafanikio kwenye mauzo bila kusahau yanatokana na kuwa na timu bora ya wanyakazi na wewe kama Mtendaji Mkuu unatakiwa kuhakikisha watu hawa wanapewa malipo na marupurupu ya kutosha. Mwandishi anatushirikisha kuwa kadri unavyopanuka kibiashara ndivyo watu wanaokuzunguka kiutendaji wanatakiwa kupanuka kwenye vipato vyao. Hali hii itakusaidia kuwa na wafanyakazi ambao wana morali ya kazi.

19. Kufanikiwa kimauzo unahitaji kuhimili figusufigisu au fitina kutoka kwa wapinzani wako wakubwa. Kuna fitina ambazo kama haupo imara zinaweza kukutoa kabisa kwenye ulimwengu wa biashara. Unahitaji kuwa imara katika kukabiliana na fitina hizo na pengine pale ambapo umetolewa nje ya mstari na wapinzani wako kibiashara inabidi uwe tayari kulipanga upya jeshi lako kwa ajili ya mapambano mapya katika soko.

20. Kuwa na uelewa mpana wa bidhaa/huduma yako na jiandae vya kutosha pale ambapo una mikutano ya kuwashawishi wateja tarajiwa kufanya biashara na wewe. Mwandishi anatushirikisha kuwa watu wengi wanakataliwa kukubaliwa kutokana na kukosa maandalizi ya kutosha juu ya kile ambacho wanakusudia kuuwauzia wateja tarajiwa. Njia pekee ya kufanikiwa kwenye eneo hili ni kuwa na uelewa wa kutosha kwenye bidhaa/huduma yako kuliko mteja unayemshawishi. Husikubali mteja tarajiwa afahamu bidhaa/huduma husika kuliko wewe kwani kufanya hivyo ni hatua ya kwanza kwako kufeli.

21. Tangeneza mpango mzuri wa kuzalisha, kufunga, kusambaza, kutangaza na kuuza bidhaa/huduma zako. Ngazi zote hizi katika uzalishaji zinahitaji ubunifu ambao umejikita kwenye kupunguza gharama za uzalishaji au uendeshaji. Hata hivyo, katika ngazi zote unatakiwa kukumbuka kuwa jambo la muhimu ni mteja aridhike na huduma au bidhaa zako. Na hapa unahitaji kuhakikisha unatimiza ahadi kwa mteja ndani ya muda husika.

22. Hakikisha fanikio moja linazaa mafanikio zaidi kwa ajili ya kufikia malengo mapana zaidi. Mwandishi anatushirikisha kuwa kadiri unavyofanikiwa ndivyo sifa zako zinavyojitangaza zaidi na hivyo kufanya mafanikio yakufuate zaidi. Kumbuka pale unapotengeneza jina kuna gharama za kuhakikisha unalinda jina lako kibiashara zaidi.

Haya ni machache ambayo nimeweza kukushirikisha kati ya mengi yaliyo kwenye kitabu hiki. Kupata nakala ya kitabu hiki BONYEZA HAPA na ujiunge na mtandao wa fikra za kitajiri kisha nitumie ujumbe wa kuomba kitabu hiki kupitia barua pepe fikrazakitajiri@gmail.com.

Niendelee kukuomba usambaze jumbe hizi kwa kadri uwezavyo ili yale unayojifunza yawafikie wengi na hatimaye tufanikiwe kuibadilisha dunia hii kuwa mahali pazuri pa kuishi (Unaposambaza makala hizi hakikisha haukopi na kupest badala yake share link). Nakutakia mapambano mema.

Karibuni kwenye fikra za kitajiri ili upate elimu isiyokuwa na mwisho.

Born to Win ~ Dream Big 

Augustine Mathias Bilondwa

Namba ya Simu:      +255 786 881 155
Mwanzilishi wa Mtandao wa 
fikrazakitajiri.blogspot.com
Barua pepe:  fikrazatajiri@gmail.com

PATA UCHAMBUZI WA KITABU CHA THE RULES OF MONEY ( KANUNI ZA PESA)
 
Mwandishi Richard Templar katika kitabu hiki ametushirikisha kanuni 107 ambazo kila mtu anaweza kuzitumia kutengeneza pesa na hatimaye kuwa tajiri. Uchambuzi wa kina wa kanuni zote (107) umeandaliwa kwa mfumo wa pdf na unapatikana kwa gharama ya Tshs. elfu tano tu (5,000/=). Kanuni zote zimechambuliwa na kuandaliwa kijitabu kidogo chenye kurasa 39 ambazo unaweza kusoma kwenye simu ya mkononi (smart phone) au kwenye kompyuta (pc).

Kupata uchambuzi wa kanuni zote tuma pesa yako kwa njia ya M-pesa au Airtel Money kupitia namba zifuatazo:-

M – Pesa tumia namba: 0763 745 451 (Majina ni Augustine Mathias)
Airtel Money tumia namba: 0786 881 155 (Majina ni Augustine Mathias)

Baada kutuma pesa hiyo nitumie ujumbe kwenye namba ya airtel (0786 881 151 451) ukiwa na barua pepe yako ili nikutumie uchambuzi wa kanuni hizi moja kwa moja kwenye mtandao wako.

UTAJIRI NI HAKI YAKO YA KUZALIWA "BEING RICH IS YOUR BIRTH RIGHT"





onclick='window.open(

Related Posts